Jumla ya Mara Iliyotazamwa

Alhamisi, 18 Aprili 2013

BI KIDUDE AFARIKI DUNIA

BI KIDUDE  ENZI ZA UHAI WAKE           
Mwanamuziki nguli wa tanzania na Afrika mashariki  Fatma Baraka Hamisi ali maarufu kama bi Kidude  amefariki dunia jana tarehe 17/04/2013 majira ya saa sita mchana akiwa nyumbani kwa ndugu zake nje kidogo ya mji wa unguja, bi kidude amefariki dunia akiwa na umri zaidi ya miaka 100 alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na uvimbe uliokuwa kwenye kongosho.
Safari ya maisha ya muziki wa bi kidude ilianza tangu akiwa na umri wa miaka 10 alianza kwa kupiga ngoma za unyago na kuimba,baadaye alianza kuimba muziki wa Pwani maarufu kama taarabu ambao ni muziki uliompa umaarufu mkubwa Tanzania na hata nje ya nchi kutokana na umaarufu huo alipata fursa ya kutembelea nchi kama vile Oman,Ufarasa, Uingereza na nyingine nyingi.
Muda mwingi alifanya muziki akiwa kwenye ziara za kuzunguka nchi za nje na alipofikisha takribani umri wa miaka 40 alirudi kufanya muziki nyumbani kwao Unguja hata hivyo kuna baadhi ya nyimbo zilizompa umaarufu mkubwa ni kama vile muogo wa jang'ombe,yalaiti na nyingine nyingi lakini katika maisha yake hakubahatika kuzaa mtoto pia bi kidude alipata elimu ya korohani tu hakubahatika kusoma elimu ya dunia.
Bi kidude amezikwa leo tarehe 18/04/2013  kijijini kwao huko unguja.
Mungu ailaze roho ya marehemu Fatma Baraka Hamisi (bi kidude) mahali pema peponi. 
Amina                 

Hakuna maoni: